WITO WA KUCHANGIA UJENZI WA HOSTEL ZA WANAFUNZI WA KIKE CHUO KIKUU MZUMBE NDAKI YA MBEYA

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera amewataka wadau mbalimbali wa maendeleo ikiwemo Taasisi za Serikali, Sekta binafsi, Wafanyabiasha pamoja na Wananchi  kuchangia harambee ya ujenzi wa hosteli za wanafunzi wa kike  Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Mbeya ambao utagharimu  Shillingi bilioni 5.8.

Akizungumza leo tarehe 25/5/2023 Mkoani Mbeya katika uzinduzi wa harambee iliyokwenda pamoja na matembezi, Mhe. Homera amesema kuwa kila mmoja anapaswa kuchangia kiasi chochote cha fedha kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa hosteli kutokana wanafunzi wa kike wanasoma katika mazingira sio rafiki.

"Vijana wetu wa kike wanakaa mtaani ambapo kuna changamoto nyingi ambazo zinawafanya wasifanye vizuri katika masomo yao, kuna vishawishi kama hawajawa  makini wanaweza kupata maradhi kutokana na mazingira wanayoishi" amesema Mhe. Homera.

Mhe. Homera amesema wananchi wa Mkoa wa Mbeya  kupitia Rasi wa  Ndaki ya Mbeya tayari  wameanza safari ya kwenda kujenga hosteli za watoto wa kike ili kuhakikisha wanasoma katika mazingira rafiki.

"Nawapongeza Chuo Kikuu Mzumbe kwa kuja na wazo hili, mimi Mkuu wa Mkoa siweze kuwaacha nitahakikisha hosteli zinakamilika na watoto wa kike  watapata hosteli  za kisasa na kuishi katika mazingira mazuri" amesema Rc Homera.

Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. William Mwegoha, amesema  lengo ni kuchangisha fedha kwa ajili ujenzi hosteli na kuwasaidia wanafunzi ili kuepukana na changamoto katika masomo yao.

Prof . Mwegoha amefafanua kuwa hatua hiyo ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais Mhe. Dkt. Samia Suruhu Hassani ambazo ameweka  mwenyewe ili kuhakikisha miundombinu ya elimu inaimalika nchini.

Ili kufikia lengo kwa wakati viongozi wa serikali, sekta binafsi, wadau wa maendeleo pamoja na wananchi kwa ujumla wanapaswa  kushiriki  harambee ya ujenzi wa hosteli  kwa kuchangia kiasi chochote cha fedha kupitia control namba 994180331310.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera akiwa katika matembezi ya hisani ya kuchangia ujenzi wa hosteli ya wanafunzi wakike 

wa Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Mbeya. Matembezi hayo yalianzia Kituo cha Basi cha Kabwe  jijini mbeya 

hadi viwanja vya ndaki hiyo eneo la Forest leo Mei 25, 2023.

Washiriki wa matembezi ya hisani ya kuchangia ujenzi wa hosteli ya wanafunzi wa kike Ndaki ya Mbeya, Chuo Kikuu Mzumbe wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ,

Mheshimiwa Juma Homera  wakati akihutumia katika harambee ya kuchangia Ujenzi wa hosteli katika ndaki hiyo leo Mei 25, 2023.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera akichangia harambee ya ujenzi wa Hosteli ya wanafunzi wa kike  wa Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya 

Mbeya jijini humo leo Mei 25,2023.  Pia amewaelezea washiriki wa hatua za kulipia  za kuchangia ujenzi kwa kumtumia  namba ya malipo 994180331310

alipotembelea  eneo zitakapo jengwa hostel hizo chuoni hapo.

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Profesa William Mwegoha akitoa taarifa ya chuo na kuelezea  umuhimu wa harambee ya ujenzi

wa Hostel ya wanafunzi wakike katika Ndaki ya Mbeya leo Mei 25, 2023.

Mwanafunzi wa  Mwaka wa Tatu Shahada ya Kwanza ya Menejimenti ya Rasilimali Watu, Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Mbeya, Neema Alex   

akielezee changamoto alizopitia alipokuwa akikaa nje ya Chuo na umuhimu wa ujenzi wa hosteli hizo  katika haramee ya ujenzi wa Hosteli za

wanafunzi wa kike Chuoni hapo leo Mei 25, 2023.

Mwanafunzi wa darasa la Tano, Shule ya Msingi Ndola Mbalizi Abubakari Shabani Mwamba   akichangia shilingi 400 katika harambee ya ujenzi wa hosteli za

Kike Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Mbeya. Na kuwaomba wananchi wa  Mkoa wa  Mbeya na vitongoji vyake kumuunga mkono Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe.

Juma Homera kwenye harambee hiyo.

Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo,(Taaluma Utafiti na Ushauri) Dkt Eliza Mwakasangula akitoa neno la shukrani kwa niaba ya

Menejimenti na wanajumuiya wa Chuo Kikuu Mzumbe.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera akizungumza  na wanajumuiya wa Chuo Kikuu Mzumbe wakati wa Harambee ya

kuchangia ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike.

Address

MBEYA CAMPUS COLLEGE
Forest Area - Mbeya City
Mzumbe University
P.O.Box  6559, Mbeya, Tanzania
Tel: +255 (0) 252502863 /57/58
Fax: +255 (0) 252502862
email: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.